Saturday 12 December 2015

Maana ya nadharia na maana ya Fasihi



Maana ya nadharia na maana ya Fasihi.
Nadharia ni mfumo wa mawazo ya kifalsafa yanayoeleza kuhusu maisha ya mwanadamu na mazingira yake.

Wamitila (2003), anaeleza kuwa nadharia ni istilahi inayotumiwa kurejelea kauli au kaida za kijumla zinazotegemezwa kwenye uwazaji fulani.

Fasihi ni sanaa ya lugha inayotumia fani mbalimbali kutolea dhamira na maudhui yanayohusu maisha ya mwanadamu.

Wamitila (2003), anasema kuwa fasihi ni kazi za kisanaa au zilizotumia lugha kwa usanii na zinazowasilisha suala fulani pamoja kwa njia inayoathiri, kugusa na kuacha athari fulani katika maisha ya binadamu.

Kulingana na Mazrui na Syambo (1992), fasihi ni utumiaji wa lugha kisanaa kutubainia utaratibu wa maisha yetu.

Wafula na Njogu (2007), wanasema kuwa nadharia ya fasihi ni mwongozo unaomwezesha msomaji wa kazi ya fasihi kuifahamu kazi ya fasihi katikatika vipengele vyake vyote.

Nadharia ya fasihi ni mfumo wa mawazo ya kifalsafa ambayo hubainisha maisha ya binadamu na mazingira yake.