MASHAIRI
Maana: - Shairi
ni utungo wa kisanaa wenye mpangilio maalum wa lugha ya mkato unaowasilisha
mawazo au ujumbe kuhusu mwanadamu au mazingira yake na
hufuata
utaratibu fulani.
Migao
ya mashairi
Mashairi huweza kugawika mara
mbili.
i)
Mashairi
huru
ii)
Mashairi
ya arudhi
Mashairi
ya arudhi
Huitwa pia mashairi ya kimapokeo.
Haya ni mashairi yanayofuata kanuni za kimapokeo au arudhi za utunzi wa
mashairi. Arudhi hizi ni pamoja na:
(i)
Kugawika
kwa shairi katika beti
(ii)
Beti
kuwa na idadi maalum ya mishororo.
(iii)
Mishororo
ya ubeti kugawika katika vipande
(iv)
Mishororo
kuwa na ulinganifu wa mizani
(v)
Shairi
kuwa na urari wa vina
(vi)
Shairi
kuweza kuimbika / kuwa na mahadhi au mapigo.
(vii)
Kuwepo
kwa kipokeo katika shairi
(viii)
Kuwa
na mtiririko wa mantiki na mawazo au muwala
(ix)
Shairi
kuwa na utoshelezo wa beti / kujisimamia kimaana.
Mashairi
huru
Pia hujulikana kama mashairi ya
kimapinduzi. Haya ni mashairi yasiozingatia lazima ya arudhi na hivyo huwa na
muundo huru. Sifa zake kuu huweza kuwa:
a) Lugha ya muhtasari
b) Lugha yenye mahadhi
c) Lugha ya kisanii iliyo na mafumbo
na taswira
d) Mara nyingine hugawika katika
beti.
e)
Mishororo
kamilifu (inayojitosheleza) na ile isiyo kamilifu (mishata)
SIFA
ZA MASHAIRI
Mashairi huwa na sifa maalum
zinazoyatambulisha kama kazi ya kishairi, yawe ya kimapokeo au kimapinduzi.
Sifa hizi ni kama vile:
1)
Mashairi
hutumia lugha ya mkato / muhtasari
2)
Ni
sanaa au kazi iliyobuniwa kwa ufundi
3)
Huwa
na mpangilio maalum kuanzia mistari hadi beti.
4) Hutumia
lugha teule na msamiati teule uliosheheni tamathali, taswira na jazanda.
5)
Mashairi
huwa na sifa ya kuweza kuimbika hivyo shairi ni wimbo na wimbo ni shairi.
Umuhimu
/ Dhima ya mashairi.
i)
Kupasha
ujumbe kwa hadhira kwa njia ya upole na
mvuto
ii) Kuelimisha na kuzindua jamii.
iii) Kuendeleza na kukuza kipawa cha
utunzi.
iv) Kuhifadhi msamiati wa lugha ya
Kiswahili na Sanaa ya fasihi.
v)
Kuburudisha
hadhira na wasomaji.
vi) Kuwasilisha hisia za ndani za mtu na mawazo
Uchambuzi
wa Mashairi
Uchambuzi au uhakiki wa shairi ni
kuvunjavunja shairi katika sehemu zake na kuzichunguza kwa makini ili kueleza ujumbe,
dhamira, maudhui na hali ya vipengee vya shairi.
Uchambuzi wa mashairi huweza
kufanywa kwa hatua.
Hatua
za uchambuzi
i.
Soma
shairi polepole na makini kupata maana ya kijumla.
ii.
Soma
shairi tena kwa utaratibu ukizingatia maneno na vipande mbalimbali na
kuchunguza maana ya kila mojawapo.
iii.
Pitia
maswali yote kwa makini ukitilia maanani aina ya majibu yanayotarajiwa.
iv.
Soma
shairi tena ukipigia mstari kwa penseli sehemu zinazoelekea kujibu maswali.
v.
Toa
majibu kamilifu kulingana na swali kwa lugha ya mtiririko.
Vipengee
vya Uchambuzi Wa Mashairi.
(i)
Anwani
– Huwa ni muhtasari wa shairi katika neno au
sentensi moja. Anwani ni kidokezo muhimu cha kinachozungumziwa katika shairi.
Anwani huweza kuwa ya moja kwa moja, fumbo, kinaya, kibwagizo au sehemu ya
kibwagizo.
Ikiwa
shairi halina anwani, basi lipewe anwani inayoafikiana na maudhui au dhamira
kwa sentensi isiyozidi maneno 6.
(ii) Maudhui – Haya ni masuala makuu au mambo
muhimu yanayohusu mwanadamu au mazingira yake yanayozungumziwa katika shairi. Kwa mfano: malezi, siasa, usalama, unyanyasaji,
ufisadi n.k
Maudhui
hung’amuliwa kwa wepesi kutokana na kisa kilichomo katika shairi.
(iii)
Dhamira / shabaha
- Ni lengo kuu
la mshairi katika kusanifu utungo wake. Dhamira ya mtunzi huwa ni ujumbe kwa
kifupi anaoutambua msomaji kutokana na mwelekeo wa usemaji wa mtunzi katika
shairi. Mfano: Baada ya kusoma
shairi, unaweza kung’amua mtunzi alitaka kusisitiza kauli kuwa uongozi
mbaya haufai, misitu ni uhai n.k.
Dhamira
hutokana na mwelekeo wa mawazo ya mshairi au falsafa yake.
(iv)
Mbinu
na tamathali za lugha -
Ni mbinu za uandishi na tamathali za usemi zilizotumiwa na mshairi katika shairi.
Mfano:
a) Mazda / ziada / zidi - kurefusha
maneno. Mfano: enda kuwa enenda.
b) Inksari / muhtasari - Ni
kufupisha maneno. Mfano: aliyefika kuwa alofika.
c)
Utohozi
– Mbinu ya kugeuza msamiati / maneno ya lugha geni ili yaandikike na kutamkika
kana kwamba ni ya Kiswahili. Mfano: Time
- taimu
One – Wani
Mbinu hii vilevile huitwa ukopaji au uswahilishaji.