Sunday 16 December 2012

Mashairi na Uchambuzi wake


MASHAIRI
Maana:  - Shairi ni utungo wa kisanaa wenye mpangilio maalum wa lugha ya mkato unaowasilisha mawazo au ujumbe kuhusu mwanadamu au mazingira yake na hufuata utaratibu fulani.

Migao ya mashairi
Mashairi huweza kugawika mara mbili.
i)                    Mashairi huru
ii)                  Mashairi ya arudhi

Mashairi ya arudhi
Huitwa pia mashairi ya kimapokeo. Haya ni mashairi yanayofuata kanuni za kimapokeo au arudhi za utunzi wa mashairi. Arudhi hizi ni pamoja na:
(i)                       Kugawika kwa shairi katika beti 
(ii)                     Beti kuwa na idadi maalum ya mishororo.
(iii)                   Mishororo ya ubeti kugawika katika vipande
(iv)                   Mishororo kuwa na ulinganifu wa mizani
(v)                     Shairi kuwa na urari wa vina
(vi)                   Shairi kuweza kuimbika / kuwa na mahadhi au mapigo.
(vii)                 Kuwepo kwa kipokeo katika shairi
(viii)               Kuwa na mtiririko wa mantiki na mawazo au muwala
(ix)                   Shairi kuwa na utoshelezo wa beti / kujisimamia kimaana.
Mashairi huru
Pia hujulikana kama mashairi ya kimapinduzi. Haya ni mashairi yasiozingatia lazima ya arudhi na hivyo huwa na muundo huru. Sifa zake kuu huweza kuwa:
a)      Lugha ya muhtasari
b)      Lugha yenye mahadhi
c)      Lugha ya kisanii iliyo na mafumbo na taswira
d)     Mara nyingine hugawika katika beti.
e)      Mishororo kamilifu (inayojitosheleza) na ile isiyo kamilifu (mishata)


SIFA ZA MASHAIRI
Mashairi huwa na sifa maalum zinazoyatambulisha kama kazi ya kishairi, yawe ya kimapokeo au kimapinduzi.
Sifa hizi ni kama vile:
1)            Mashairi hutumia lugha ya mkato / muhtasari
2)            Ni sanaa au kazi iliyobuniwa kwa ufundi
3)            Huwa na mpangilio maalum kuanzia mistari hadi beti.
4)       Hutumia lugha teule na msamiati teule uliosheheni tamathali, taswira na jazanda.
5)            Mashairi huwa na sifa ya kuweza kuimbika hivyo shairi ni wimbo na wimbo ni shairi.

Umuhimu / Dhima ya mashairi.
i)        Kupasha ujumbe  kwa hadhira kwa njia ya upole na mvuto
ii)      Kuelimisha na kuzindua jamii.
iii)    Kuendeleza na kukuza kipawa cha utunzi.
iv)    Kuhifadhi msamiati wa lugha ya Kiswahili na Sanaa ya fasihi.
v)      Kuburudisha hadhira na wasomaji.
     vi)  Kuwasilisha hisia za ndani za mtu na mawazo

 Uchambuzi wa Mashairi
Uchambuzi au uhakiki wa shairi ni kuvunjavunja shairi katika sehemu zake na kuzichunguza kwa makini ili kueleza ujumbe, dhamira, maudhui na hali ya vipengee vya shairi.
Uchambuzi wa mashairi huweza kufanywa kwa hatua.
Hatua za uchambuzi
i.                    Soma shairi polepole na makini kupata maana ya kijumla.
ii.                  Soma shairi tena kwa utaratibu ukizingatia maneno na vipande mbalimbali na kuchunguza maana ya  kila mojawapo.
iii.                Pitia maswali yote kwa makini ukitilia maanani aina ya majibu yanayotarajiwa.
iv.                Soma shairi tena ukipigia mstari kwa penseli sehemu zinazoelekea kujibu maswali.
v.                  Toa majibu kamilifu kulingana na swali kwa lugha ya mtiririko.

Vipengee vya Uchambuzi Wa Mashairi.
(i)                 Anwani  – Huwa ni muhtasari wa shairi katika neno au sentensi moja. Anwani ni kidokezo muhimu cha kinachozungumziwa katika shairi. Anwani huweza kuwa ya moja kwa moja, fumbo, kinaya, kibwagizo au sehemu ya kibwagizo.
          Ikiwa shairi halina anwani, basi lipewe anwani inayoafikiana na maudhui au dhamira kwa                      sentensi isiyozidi maneno 6.

(ii)        Maudhui – Haya ni masuala makuu au mambo muhimu yanayohusu mwanadamu au mazingira yake yanayozungumziwa katika shairi. Kwa mfano: malezi, siasa, usalama, unyanyasaji, ufisadi n.k
                         Maudhui hung’amuliwa kwa wepesi kutokana na kisa kilichomo katika shairi.

(iii)             Dhamira / shabaha - Ni lengo kuu la mshairi katika kusanifu utungo wake. Dhamira ya mtunzi huwa ni ujumbe kwa kifupi anaoutambua msomaji kutokana na mwelekeo wa usemaji wa mtunzi katika shairi. Mfano: Baada ya kusoma shairi, unaweza kung’amua mtunzi alitaka kusisitiza kauli kuwa uongozi mbaya haufai, misitu ni uhai n.k.
                        Dhamira hutokana na mwelekeo wa mawazo ya mshairi au falsafa yake.

(iv)       Mbinu na tamathali za lugha - Ni mbinu za uandishi na tamathali za usemi zilizotumiwa na mshairi  katika shairi.
            Mfano:
a)      Mazda / ziada / zidi - kurefusha maneno.    Mfano: enda kuwa enenda.
b)      Inksari / muhtasari - Ni kufupisha maneno. Mfano: aliyefika kuwa alofika.
c)      Utohozi – Mbinu ya kugeuza msamiati / maneno ya lugha geni ili yaandikike na kutamkika kana kwamba ni ya Kiswahili.         Mfano: Time - taimu
               One  – Wani
                                  Mbinu hii vilevile huitwa ukopaji au uswahilishaji.






28 comments:

  1. Replies
    1. Shukrani kwa pongezi zako. Na tukitukuze Kiswahili katika fani zake zote. Wa aleikum salaam.

      Delete
    2. asante sana kwa kuweza kutoa na kutuelimisha kwa njia ya urahisi

      Delete
  2. Ahsante sana kaka kwa kutupasha haya..mola akuzidishie

    ReplyDelete
  3. Fazuul edwin .Napend kazi hio

    ReplyDelete
  4. Enter your comment...napenda kazi hio

    ReplyDelete
  5. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete
  6. nimeipenda sana.bravoh kwa wanakiswahili

    ReplyDelete
  7. Asante umenijuvya kiswahili kitukuzwe

    ReplyDelete
  8. mda mwingine mtoe maana ya ushairi pendwa

    ReplyDelete
  9. Sands Casino | New Jersey online casino
    The 마카오 샌즈 카지노 Sands Casino is located on the beach in the Marina District. The casino is located in the Ocean Sound area, just a few minutes from Borgata

    ReplyDelete
  10. Tofauti kati ya shairi huru na arudhi

    ReplyDelete
  11. Kazi hii iko poa sana👩‍🚒👩‍🚒👩‍🚒

    ReplyDelete
  12. Mashallah
    (Saja DEBRIGE)

    ReplyDelete
  13. Asante sana kwa kazi hii

    ReplyDelete
  14. Kazi njema sana

    Naomba utueleze pia istilahi za ushairi

    ReplyDelete
  15. Asante sa a

    ReplyDelete
  16. My God bless your work.

    ReplyDelete